Waziri wa Nishati na Madini akutana na Rais wa Kampuni ya Chiyoda Corporation ya Japan - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Waziri wa Nishati na Madini akutana na Rais wa Kampuni ya Chiyoda Corporation ya Japan


Waziri wa Nishati na Madini, Mh.Profesa Sospeter M. Muhongo, akimfafanulia jambo Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Chiyoda Corporation ya Japan, Bw. Shogo Shibuya. Waziri Muhongo alikutana na Bw. Shogo kwa lengo la kufanya mazungumzo kuhusu uwekezaji nchini kwenye miradi ya uzalishaji wa umeme kwa kutumia jua pamoja na ujenzi wa miundombinu ya usindikaji wa gesi asilia na mitambo ya kuzalisha umeme. Mkutano huo ulifanyika mjini Yokohama, Japan wakati wa Mkutano wa tano wa Kimataifa wa Tokyo unaojadili Maendeleo ya Afrika (Tokyo International Conference on African Development (TICAD V) uliohudhuriwa na Wakuu wa nchi za Afrika na Japan pamoja na Mawaziri na Maofisa wa Serikali hizo. Mkutano ulifanyika tarehe 1 hadi 3 Juni, 2013.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages