Taarifa Maalum Kutoka Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Juu ya Kufungwa Kwa Sehemu ya Barabara ya Kontena,Kanisani-Msikitini hadi Changanyikeni - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Taarifa Maalum Kutoka Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Juu ya Kufungwa Kwa Sehemu ya Barabara ya Kontena,Kanisani-Msikitini hadi Changanyikeni

UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM OFFICE OF THE DEPUTY VICE-CHANCELLOR (ADMINISTRATION)
P.O. BOX 35091 - DAR ES SALAAM - TANZANIA 
.
Tel.:    022 2410500 - 8 Ext.
2003

           022 2410394 - Direct Line
Fax:    022 2410718
Ref:     z1/18
Telegram:  University of Dar es Salaam
E-mail:    dvc-pfa@admin.udsm.ac.tz
Website:   www.udsm.ac.tz 
21  Juni, 2013  
Wanajumuiya Wote

YAH: KUFUNGWA KWA SEHEMU YA BARABARA YA KONTENA—KANISANI/MSIKITINI— CHANGANYIKENI 

Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam unautaarifu umma kuwa kipande cha barabara kuanzia kumbi za mihadhara ya Yombo 1&2 na Bweni Na. 6 hadi barabara ya Changanyikeni kitafungwa kuanzia Jumapili tarehe 23 Juni 2013.

Barabara inayoanzia kituo cha daladala cha Kontena hadi Bweni Na. 6 ilitengenezwa kwa ajili ya matumizi ya ndani ya Chuo tu, ingawa kwa siku za karibuni matumizi ya barabara hiyo yameongezeka kiasi cha kuhatarisha usalama wa wanafunzi na wafanyakazi wanaotumia kumbi za mihadhara na ofisi zilizopo maeneo hayo.

Kwa hiyo, watu wote waliozoea kutumia barabara hiyo kuelekea Changanyikeni kwa vyombo vya usafiri vya moto, wanashauriwa kutumia barabara ya kawaida inayoanzia au kutokea karibu na tawi la NBC.

Tunawapa pole kwa usumbufu utakaojitokeza kwa kufungwa kwa barabara hiyo.

Prof. Y. D. Mgaya
NAIBU MAKAMU MKUU WA CHUO - UTAWALA

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages