WATANZANIA WASHINDWA KUFANYA VIZURI KIPINDI CHA TANO CHA GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

WATANZANIA WASHINDWA KUFANYA VIZURI KIPINDI CHA TANO CHA GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE

01Washindi wa kipindi cha tano cha Guinness Football Challenge Ken Muturi (kushuto) na Chris Mwamgi(kulia) wakishangilia ushindi walioupata huku wakiwa wamebeba pesa taslimu walizojishindia katika shindano hilo jana usiku na pembeni ni mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho Lary Asengo(anayepiga makofi kulia).
 ………………………………………………..
 Jana usiku kupitia Televisheni za ITV na Clouds TV timu ya Tanzania ilishindwa kutumia nafasi ya kipindi cha mwisho cha mashindano ya “Guinness Football Challenge” katika hatua ya Afrika Mashariki baada ya kutolewa na timu kutoka Kenya. Rangi nyekundu imeonekana kuwa ni rangi ya bahati kwa timu za Kenya kwani hii ni timu ya nne kutoka Kenya kufanikiwa kufuzu kuingia hatua ya Pan-African GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGETM. Kenneth Mukuri na Chris Mwamgi ndio walioibuka washindi jana usiku kwani walifanikiwa kufika katika hatua ya mwisho ya kulenga ukuta  wa pesa wa Guinness ambapo walijishindia dola za kimarekani  1,500. 

 Ni vipi Kenneth na Chris wataweza kumudu hatua ya Pan-African? Sasa wana nafasi ya kuiwakilisha nchi yao katika mashindano ya Pan-African ambapo watakutana na wawakilishi pekee kutoka Tanzania, Daniel Msekwa na Mwalimu, washiriki kutoka Uganda Alex Muyobo na Ibrahim Kawoova pamoja na wenzao kutoka Kenya,Francis Ngigi na Kepha Kimani(washindi wa kipindi cha 2), Kenneth Kamau na Wills Ogutu(washindi kipindi cha 3) na Ephantus Nyambura na Samuel Papa(washindi kipindi cha 4).
 Timu hizi tano zitakua uwanjani kutimiza malengo yao, ambapo watakutana uso kwa uso na washiriki kutoka Ghana na Cameroun kuonesha ni nani ana maarifa zaidi na ujuzi wa kusakata kabumbu,  hata kuvishwa ubingwa wa Pan-African na  kuondoka na dola za kimarekani 250,000.
 
 Usikose kuangalia mashindano haya kupitia televisheni za ITV na Clouds TV huku ukiburudika na kinywaji cha GUINNESS.
 
                              Tafadhali kunywa kistaarabu – Hairuhusiwi kwa wenye umri chini ya miaka 18.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages