Darasa la saba sasa kujiunga vyuo vikuu - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Darasa la saba sasa kujiunga vyuo vikuu

Jengo la Chuo Kikuu Dodoma(Udom) moja ya vyuo vitakavyo tumika katika utaratibu huo mpya 

Udahili huo utakaoanza mwaka huu wa masomo 2013/14, utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la saba na kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi ya chuo kikuu.

Na Ibrahim Yamola, Mwananchi.
 
Dar es Salaam. Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU), imepanga kuanza kuwadahili wanafunzi wa kujiunga na masomo ya vyuo vikuu kwa kutumia uzoefu wao.
Udahili huo utakaoanza mwaka huu wa masomo 2013/14, utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la saba na kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi ya chuo kikuu.
Kupitia utaratibu huo mpya, mtahiniwa atajiunga na Chuo Kikuu kulingana na fani atakayoiomba na atatakiwa kufanya mitihani mitatu na kufaulu kwa wastani wa daraja B.
Mkurugenzi wa Ithibati na Ubora wa Elimu ya Juu kutoka TCU, Dk Savinus Maronga aliliambia gazeti hili kuwa baada ya kuona kuna watu wengi wanaopenda kuendelea na masomo ya elimu ya juu, lakini wameshindwa kutokana na kutokuwa na vigezo, TCU imeamua kuanzisha mitihani hiyo maalumu. Alisema kuwa mfumo huo unaojulikana kama ‘Recognition of Prior Learning’ (RPL), utamwezesha mwombaji kudahiliwa vyuoni kupitia tume hiyo kama wanavyofanya watahiniwa wengine.
Sifa zinazotakiwa

Kuhusu sifa za kujiunga, Dk Maronga alisema kuwa mwombaji anatakiwa kuwa na umri kuanzia miaka 25 na kuendelea, sambamba na kuwa na elimu isiyopungua darasa la saba.

“Mwombaji anatakiwa kuwa na nia ya kujiunga na elimu ya chuo kikuu na uzoefu wa kile ambacho anakusudia kukisoma.
Awe na uwezo wa kuandika na kusoma Lugha ya Kiingereza, ambayo ndiyo inayotumika kufundishia vyuoni,”alisema Dk Maronga na kuongeza:
“Kuna watu wameishia darasa la saba, lakini wamefanya kazi katika eneo moja, mfano karani wa mahakama, mwandishi wa habari kwa muda mrefu. Hivyo mfumo huu utawawezesha kuendelea na masomo bila tatizo.”
Vigezo
Mkurugenzi huyo alisema, kutakuwa na mitihani ya masomo matatu, ambayo mtahiniwa ili apate nafasi ya kuendelea na masomo ni lazima afaulu kwa wastani wa daraja B.

Alisema daraja la kwanza linaloanza na alama A ni 75-100, daraja B+ ni 60-75, B ni 50-59, C ni 40-49, D ni 35-39 na daraja E ni 0-34.
“Katika mitihani mitatu atakayoifanya, atatakiwa kupata wastani wa daraja ‘B’ na somo husika la fani yake atatakiwa kupata alama B ili kuwa na vigezo vya kupata cheti kitakachomwezesha kuendelea na masomo yake,”alisema Dk Maronga.

Source: Mwananchi

1 comment:

  1. Anonymous9:58 AM

    !MIMI NI KIJANA MWENYE UMRI WA MIAKA 29 NILIMALIZA DARASA LA SABA MWAKA 1999 KWA BAHATI MBAYA NILISHINDWA KUENDELEA NA ELIMU YA SECONDARY KULINGANA NA AZAZI WANGU KUTOKUWA N UWEZO .NILIKAA NYUMBANI MIAKA 9 NIKITAFUTA FEDHA YA KUJISOMESHEA LAKINI MUNGU AKANISADIA NIKAPATA KIBARUA YA KUFANYA NIKATAFUTA CHUO CHA UFUNDI YA ELECTRONICS & NA COMPUTER NIKA APPLY PALE MIAKA MIWILI 208-2010 NILPO MALIZA NIKAJIAJIRI KWA KAZI
    ZA KIUFUNDI NDANI YA MDA MFUPI TENA NIKITAFUTA ADA YA KUJIUNGA NA QT BAADA YA MDA NIKAJIUNGA NA QT MWAKA 2011 MUNGU AKANISAIDIA NIKAFALU KUJIUNGA NA PC 2012 NIKAANZA MASOMO YA KIDATO CHA NNE NKAFANYA MTIHANI MWAKA JANA ,LAKINI MATOKEO YANGU HAYAKUJA VIZURI YA KUNIRIZISHA MIMI NIENDELEE TENA HAPO NIKAISHIWA NA NGUFU YA KUENDELEA NA MASOMO TENA .LAKINI NILIPO ONA NAFASI NILIFURAHI SANA KWANI NATAKA NIENDELEE NA MASOMO YA FANI NILIOKWISHA CHUKUA NA JE NITAWAPATAJE ?MNIPE MWELEKEO VIZURI
    E-MAIL YANGU NI aminielimollel@yahoo.com nijibu kwa kutumia hii aaddress yangu asande

    ReplyDelete

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages