EPIQ STARS KUWASHA MOTO MAISHA CLUB DAR IJUMAA HII - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

EPIQ STARS KUWASHA MOTO MAISHA CLUB DAR IJUMAA HII

Ziara ya kuzindua nyimbo za wasanii walioshiriki shindano la kuimba la Epiq BSS itaendelea tarehe 1 mwezi wa tatu, ijumaa hii katika ukumbi wa Maisha Club Dar ambapo wasanii wote walioingia kumi bora wanatarajiwa kufanya show kali siku hiyo.

Wasanii hao ambao wiki iliyopita walifanya show kali katika ukumbi wa Maisha Club Dodoma, wanatarajiwa pia kufunika Maisha Club. Wasanii hao ambao wengi wamekuwa wakisubiriwa kwa hamu na wengi tokea shindano lilipoisha mwishoni mwa mwaka jana wamekuwa wakizungumziwa na wengi kama wanamziki watakaofanya vizuri mwaka huu. Wasanii
watakaofanya show Dar ni Menina Atick, Nsami Nkwabi, Nshoma, Vincent, Husna Nassor, Geofrey Levis, Wababa Mtuka, Norman Severino pamoja na mshindi wa milioni hamsini, Walter Chillambo.
Huku baadhi ya nyimbo zikiwa tayari zinafanya  vizuri kwenye soko la muziki kama wimbo mpya wa Walter-Siachi, Menina-Dream Tonight, Husna-Nawamimina, Wababa-My Wife na Nsami- Muongo usiku huo pia utakuwa na vitu vipya kibao, pamoja na uzinduzi wa nyimbo mpya za Norman, Nshoma, Vincent na Godfery.

Akizungumzia show hiyo,mmoja wapo wa wasanii hao, Walter anasema wapenda burudani wa Dar wasikose kuja kumshuhudia yeye na wasanii wengine wa Epiq BSS wakifanya vitu vyao kwani wamejipanga kwa muda mrefu.

‘Pamoja na wimbo wangu wa Siachi pia mashabiki watapata fursa ya kuusikia wimbo wangu utakaoufuata siku hiyo hiyo’ alisema Walter, ambaye alifanya show kali sana Dodoma. Usiku huo pia utapambwa na burudani kali kutoka kwa wakali wengine kama Ben Paul, Barnaba, Linah na Rich Mavoko.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages