……………………………………….
Na Tiganya Vincent-MAELEZO-Dar salaam
Ujerumani imetoa jumla ya shilingi bilioni 352( euro milioni
176) kwa Tanzania kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za
maendeleo katika kipindi miaka mitatu ijayo.
Makubaliano ya msaada huo
yamesaini leo jijini na Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa kwa upande
wa Tanzania na Balozi wa Ujerumani nchini Kluas Peter Brandes. Akizungumza mara baada ya kusaini
makubaliano hayo kwa niaba ya Tanzania Waziri wa Fedha dr. Mgimwa
alisema kuwa fedha hizo zitasaidia shughuli mbali za maendeleo katika
kipindi cha mwaka 2012/13- hadi 2014/15.
Alisema kuwa msaada huo unalenga
maeneo ya kuboresha utawala bora katika serikali za mitaa, kusaidia
sekta ya afya , nishati , maliasili, maji, na kuboresha programu ya
usimamizi wa fedha za umma.
Dr. Mgimwa aliongeza kuwa eneo
jingine ambapo hizo zitaelekezwa ni pamoja na kusaidia mfuko wa bajeti
kwa kipindi miaka mitatu hiyo na kusaidia ofisi ya Taifa ya Mkaguzi wa
hesabu za serikali . Alisema kuwa miradi hiyo itasaidia
kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini
(MKUKUTA) na hivyo kuboresha hali ya uchumi na kijamii ya wananchi.
Aidha Waziri huyo wa Fedha
alimuhakikisha Balozi wa Ujerumani nchini kuwa , Serikali itahakikisha
fedha za msaada zinatuma katika maeneo yalipangwa kwa manufaa ya
wananchi ili matokeo yake yaweze kuonyesha thamani ya fedha waliyotoa.
Naye Balozi Brandes alisema kuwa
Nchi yake itaendelea kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu na Tanzania
ili kufikia malengo ya kupambana na umaskini na hivyo kuboresha maisha
ya Watanzania hasa waishio vijijini. Aliongeza kuwa msaada waliotoa
utasaidia wakazi wa mijini kupata maji safi na salama kwa ajili ya
kujikinga na magonjwa yatokanayo na maji yasiyo salama.





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)