Meneja
wa Kinywaji cha Kilimanjaro Bw. George Kavishe akizungumza na
waandishi wa habari, katika mkutano uliofanyika katika ofisi za
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania TFF wakati kampuni ya bia
ya TBL ilipokabidhi vifaa vya michezo kwa timu za Simba na Yanga,
tayari kwa kuanza mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom inayotarajiwa
kuanza Jumamosi Januari 20 2012.
Kutoka
kulia ni Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah, Steven Kilinde Mkurugenzi
wa Mahusiano TBL, George Kavishe Meneja wa kinywaji cha Kilimanjaro,
Evodius Mtawala Katibu Mkuu wa Simba na Boniface Wambura Msemaji wa TFF
wakionyesha vifaa vilivyokabidhiwa ka timu ya Simba.
Mkurugenzi wa Mahusiano wa kampuni ya bia ya Serengeti Steven Kilinde akikabidhi jezi kwa Katibu Mkuu wa timu ya Yanga Selestine Mwesigwa
katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika ofisi za Shirikisho
la mpira wa miguu nchini Tanzania leo katikati ni Meneja wa Kinywaji
cha Kilimanjaro Bw. George Kavishe na kushoto ni Katibu Mkuu wa TFF
Angetile Osiah.
Kutoka
kushoto ni Mkurugenzi wa Mahusiano wa kampuni ya bia ya Serengeti
Steven Kilinde, Meneja wa Kinywaji cha Kilimanjaro Bw. George Kavishe,
Katibu Mkuu wa timu ya Yanga Selestine Mwesigwa
na kushoto ni Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah wakionyesha vifaa
vilivyokabidhiwa kwa timu ya Yanga katika hafla ya makabidhiano
iliyofanyika katika ofisi za Shirikisho la mpira wa miguu nchini
Tanzania leo.
Viongozi
wa Yanga na Simba pamoja na TBL wakiwa katika picha ya pamoja baada ya
makabidhiano ya vifaa vya michezo kwa timu ya Simba na Yanga. 




No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)